user avatar
Mo Dewji Foundation
@DewjiFoundation
Founded by @moodewji, we work to improve the lives of Tanzanian citizens through health, education and community development.
Tanzania
Joined April 2014
Posts
  • Pinned
    user avatar
    Wiki hii, kwa ushirikiano na Shule ya Kimataifa ya Al Muntazir, tulishiriki matembezi ya hisani ili kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa Usonji, yaliyohudhuriwa na Naibu Waziri Mkuu, Mh. Dkt. Dotto Biteko. Tutaendelea kushirikiana na wadau wenzetu kujenga Tanzania yenye afya bora.
  • user avatar
    “I thank Allah that I have returned home safely. I thank all my fellow Tanzanians, and everyone around the world for their prayers. I thank the authorities of Tanzania, including the Police Force for working for my safe return.” — Mohammed Dewji (3:15AM, Dar es Salaam)
  • user avatar
    Familia ya Dewji imetangaza zawadi ya Tsh. Bilioni Moja kwa mtu yeyote ambaye atatoa taarifa ambazo zitawezesha kupatikana kwa Mohammed Dewji. Mwenye taarifa anaweza kuwasiliana na mwanafamilia Murtaza Dewji kwa namba 0755030014, 0717208478 na 0784783228 na [email protected]
  • user avatar
    Tumefanya mawasiliano na Ndugu Abasi, tunafanya kinachowezekana kuhakikisha anapata matibabu.
  • user avatar
    Taasisi inafanya mawasiliano na familia kuangalia ni kwa namna gani tunaweza kusaidia🙏🏾
    Asha Adam Issa Mwanafunzi, Babati vijijini. Amepatwa na uvimbe begani kama anavyoonekana. Walimpeleka hospitali mkoa Manyara akapewa rufaa Haydom. Haydom wamempa rufaa Muhimbili. Wazazi hali ngumu. Wameshindwa kwenda Muhimbili. Wanaomba msaada. Simu ya mzazi 0683203363 @moodewji
  • user avatar
    Leo ni siku ya kuzaliwa ya mwanzilishi wa taasisi yetu Bw. Mohammed Dewji. Tunakuombea afya njema na baraka. Tunakushukuru kwa moyo wako wa huruma kwa kujitoa katika kuwajali watu wanaoishi katika hali ngumu na wanaopitia changamoto mbalimbali.
  • user avatar
    Update: Tumefanikiwa kuwasiliana na mama wa mtoto, tutawasafirisha kutoka Mbeya mpaka Dar pamoja na kugharamia matibabu wakiwa hospitali ya Muhimbili.
  • user avatar
    “Namshukuru Mwenyezi Mungu nimerudi salama nyumbani. Nawashukuru Watanzania wenzangu na watu wote kote duniani kwa dua na sala zao. Nashukuru mamlaka zote, ikiwemo Jeshi la Polisi, zilizofanya kazi ya kuhakikisha narudi salama.” — Mohammed Dewji (Saa 9:15 alfajiri, Dar es Salaam)
  • user avatar
    Familia ya Dewji inawakaribisha wanahabari kutoka vyombo vyote vya habari katika mkutano utakaofanyika leo saa 6:30 mchana katika ofisi za kampuni ya MeTL Group zilizopo katika jengo la Golden Jubilee Towers ghorofa ya 20 mtaa wa Ohio, Posta jijini Dar es Salaam.
  • user avatar
    TAARIFA YA MAOMBI: tunakaribisha wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza kuomba Udhamini wa Programu ya Mo ambao unalipia gharama za Chuo, gharama za awali za kujiandikisha, malazi na chakula. Kwa maelezo zaidi juu ya uombaji bonyeza link (kiunganishi) iliyo kwenye kurasa yetu.
  • user avatar
    Pamoja na @SimbaSCTanzania, tuliwatembelea na kuwapa zawadi mbalimbali watoto waliopo katika mahabusu ya watoto, iliyopo Upanga, Dar es Salaam.
  • user avatar
    Leo Mungu ametujaalia kuwatembelea na kutoa Sadaka kwa watoto Yatima na wenye uhitaji katika vituo 7. Tunaikumbusha jamii kuendelee kuwasaidia wahitaji kwenye jamii yetu.
  • user avatar
    Hawa ni wanafunzi wapya wa Programu ya Mo, ambao wanatokea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)! Tuna furaha kuwa nao na tunawatakia kila la kheri katika masomo yao 💪
  • user avatar
    Leo tumewakaribisha baadhi ya wanafunzi wapya wa program ya Mo Scholars. Tunafurahi kuwa nao kuanzia mwanzo wa mbio za kufanikisha ndoto zao. Bado tupo kwenye mchakato wa kuhakiki maombi na kuwahoji wanafunzi. Kwa hivyo kwa wanaosubiri majibu, yatatoka wiki chache zijazo.